

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema kutokana na upekee wa Bima ya Afya kwa Wote, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha wamependekeza baadhi ya vyanzo vya mapato vya kuendesha mfuko huo.
Vyanzo hivyo ni pamoja na sehemu ya mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vikali,
bidhaa za vipodozi, kodi ya michezo ya kubahatisha, ada ya Bima za vyombo vya moto na mapato yatokanayo na ushuru wa miamala ya kielektroniki kwa kadiri itakavyopendekezwa na Waziri mwenye dhamana na masuala ya fedha, fedha zitakazotengwa na Bunge, mapato yatokanayo na uwekezaji wa mfuko na zawadi
pamoja na misaada kutoka kwa wadau mbalimbali.
Waziri Ummy ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ambao ulikwama mwezi Februari mwaka huu kwa hoja iliyotolewa na Bunge ya kutokuwepo kwa chanzo endelevu cha fedha za kutekeleza mpango huo.
SALALI:Tunampongeza Rais Samia Kwa Kujumuisha Watu Wenye Ulemavu Dira 2050.
Rais Samia Azindua Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050, Asisitiza Utekelezaji Wa Vitendo Na Upimaji Wa Matokeo
UFUGAJI WA SAMAKI KWA KUTUMIA NJIA YA KISASA UMEONGEZEKA.
WATENDAJI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 WAFUNDWA
AJIRA ZA MOJA KWA MOJA KATIKA SEKTA YA UTALII ZIMEONGEZEKA.
IDADI YA WATALII WA NDANI WALIOTEMBELEA MKOA WA TABORA IMEONGEZEKA.
AJIRA ZA MOJA KWA MOJA KATIKA SEKTA YA UTALII ZIMEONGEZEKA.
eGA Yaonesha Namna Serikali Inavyotekeleza Mageuzi Kidigitali kwenye Maonesho ya sabasaba.
DKT. YONAZI AONGOZA KIKAO CHA TANZANIA NATIONAL COORDINATING MECHANISM (TNCM)
Uzalishaji wa Madini Umeongezeka kutoka Tani 7.9 Hadi Tani 42.5