BETTING kuchangia Bima ya Afya kwa Wote | The Dodoma Post
The Dodoma Post Siasa

BETTING kuchangia Bima ya Afya kwa Wote

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema kutokana na upekee wa Bima ya Afya kwa Wote, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Wizara ya Fedha wamependekeza baadhi ya vyanzo vya mapato vya kuendesha mfuko huo.

Winner Marawiti
By Winner Marawiti
01 Nov 2023
BETTING kuchangia Bima ya Afya kwa Wote

Vyanzo hivyo ni pamoja na sehemu ya mapato yatokanayo na ushuru wa bidhaa kwenye vinywaji vyenye kaboni, vinywaji vikali,
bidhaa za vipodozi, kodi ya michezo ya kubahatisha, ada ya Bima za vyombo vya moto na mapato yatokanayo na ushuru wa miamala ya kielektroniki kwa kadiri itakavyopendekezwa na Waziri mwenye dhamana na masuala ya fedha, fedha zitakazotengwa na Bunge, mapato yatokanayo na uwekezaji wa mfuko na zawadi
pamoja na misaada kutoka kwa wadau mbalimbali.

Waziri Ummy ameyasema hayo Bungeni jijini Dodoma wakati akiwasilisha Muswada wa Bima ya Afya kwa Wote ambao ulikwama mwezi Februari mwaka huu kwa hoja iliyotolewa na Bunge ya kutokuwepo kwa chanzo endelevu cha fedha za kutekeleza mpango huo.

WATENDAJI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 WAFUNDWA

WATENDAJI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 WAFUNDWA

CHIPUKIZI ACHUKUA FOMU YA UDIWANI KATA YA MWEMBESONGO.

CHIPUKIZI ACHUKUA FOMU YA UDIWANI KATA YA MWEMBESONGO.

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

Maiko Salali Arejesha Fomu ya Kugombea Ubunge Jimbo la Mpwapwa, Apongeza CCM kwa Ujumuishwaji wa Makundi Maalum

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

DWIGHT DANDA KIJANA MDOGO NA MHITIMU WA CHUO KIKUU ATIA NIA UBUNGE KIBAMBA

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma

Katimba aomba ridhaa Ubunge viti maalumu Kigoma